Iko hivi......ukoloni ulipokufa ulibaki ukoloni mamboleo. Ukimuoa single mother lazima atadate na baba watoto anytime. Labda uhame au uwatenganishe kwa kuuwa mmoja
 
Waswahili wanasema huwezi zuia mafuriko kwa mikono, kama huyo single madha aliachana na mpenzi wake kwa kigezo chochote nje na mgogoro wa kimapenzi jua tu at some point watafanya yao tu. Japo si wanawake wote wenye akili za kijinga.

Ishu kama kuachana kwa sababu ya ugumu wa maisha, Baba mtoto akishaimarika kiuchumi lazima muwe mnashea mke kinamna flani!

Nina shemeji yangu ambaye ye ameamua ku control hio situation kwa kuwa ana meet na jamaa anytime ambapo atakuwa anahitaji kumuona mtoto na huwa anampeleka yeye personally so sister hana nafasi ya kuonana na mzazi mwenzie. Nadhani ndio option nzuri zaidi
 
Kiuhalisia hiki kitu ilichokuja nacho hakitekelezeki...
 
Hakuna mwanaume anaweza toa pesa ya Matumizi bila kupewa utamu na mama watto wake japo wameachana.. wamama wachache sana wanaweza kukazaa
 
Kwani hao ambao hawajazaa wapo kizazi hiki?
Ni almost 70 ya wanawake walio katika umri wa kuolewa Wana watoto tayari.

Na wao wanasali kila siku wapate ndoa za "mume wa peke yao"
Baada ya hapo yeye anaanza kumtumikia na baba wa mtoto.
Ni Bora uendelee kuzaa tu ukiishi kwenu au ueleweke kuwa wewe unaishi peke yako kuliko kumtesa mtu mwingine
 
Weka na za walioolewa na single fathers
 
Nikweli, sikuhizi wanawake wanawahi kuzaa kwanza, cha ajabu wanaume wenyewe ndo wanaharibu hawatimizi lengo anaenda kuoa asiyezaa anaacha huyu anajilalamikia pekeake, tatizo lipo kwa wanaume
 
pole sana mkuu kwa kuwa kipofu mbele ya single maza
ni issue ya muda tu, yakikukuta madhira huko usiache kutuletea mrejesho

Mkuu usinipangie mwanamke wa kuoa asee huna mamlaka hayo.
Mbona tunawaona ambao hawajazaa bado wanawasumbua sana wanaume zao
 
Hiyo assumption yako ni ya kitoto na wala hujafanya utafiti wa kutosha kuhusu hili.
Kwanza nikuulize, jee hawa wanawake wameonjwa na kuzalisha na nani?
Jee matatizo mengi ya ndoa hivi sasa yanatokana na wanawake ambao in single mamas? Au wale ambao mnaona kuwa hawajaonjwa [kwa vile hawana watoto].
Suala la kuoa ni maamuzi ya wawili bila kujali mazingira ambayo wametokea.
Mfano mzuri ni mimi mwenyewe.
kwanza mimi ni mtoto wa dar [nadhani unaelewa maana yangu]
pili- nilichelewa sana kuoa[inawezekana kutokana na utundu mwingi ]
Nilioa miongo miwili sasa na mwanamke niliyomuoa aliwahi kuolewa na alikuwa na watoto.
Wakati ninafanya maamuzi ya kuoa, wale wote walionitakia mema walipinga sana.
Kuna wengine walidiriki hata kunitafutia warembo hasa[simba anapenda kuwinda mwenyewe]
Ukweli nilitekeleza azma yangu nikaoa na baadaye wale watoto wakataka waje kuishi na mama yao[sikuwa na kizuizi]. Niliwalea watoto wale na wote wamemaliza chuo kikuu kuna wengine wameshaolewa.
Mke wangu, wangu amekuwa msuluhishi wa ndoa nyingi za rafiki zangu na katika kipindi chote hiki sijajuta uamuzi wangu wa kumuoa.
Kuna wakati mwingine huwa ninatania kuwa hata tukifa na huko kuzimu kama nitaulizwa nataka mke wa aina gani, bado nitamchagua huyu niliyo naye.
 
Utakuwa na tatizo mkuu. Yaani ulioa mwanamke mwenye watoto 2 huku were ukiwa huna? Kwann usichukue mdada ambaye hana mtoto?

Bila shaka ulilazimika kumuoa huyo singo mama kwa kuwa ulichelewa kuoa hivyo umri ulikuwa umeenda sana halafu ulikuwa huna hela, hivyo wasichana walikuwa wanakukataa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…