Kuoa Single Mama ni sawa na kunywa soda iliyofunguliwa na kuonjwa
Habari za weekend wakuu?
Kwanza kabisa bandiko hili halihusiani na wale wanaume ambao sio wawajibikaji wanaokwepa majukumu yao wakishawazalisha wanawake na halihusiani na wanawake waliozalishwa na waume za watu(hii inaitwa single mother by choice).

Kuna mambo yanahuzunisha sana kwenye jamii zetu ikiwemo hili wimbi la dada zetu/ wanawake kuzalishwa bila ya ndoa na kuachwa. Kuna muda wanaume tunabebeshwa lawama kuhusu hali hii kwa kuwaacha ambao tumewazalisha na kuoa wanawake wengine lakini chanzo kikubwa ni wao wenyewe.
Kwa hali niliyoishuhudia ni dhahiri single mothers watazidi kuongezeka kila uchwao. Kuna dada(huyu sio shemeji jamaa hataki kabisa nimwite shemeji) kazalishwa na jamaa yangu (wapo mikoa tofauti), huyu jamaa bado mambo sio freshi ila anajitahidi sana kumhudumia mwanae na huyu dada kwa kumlipia kodi, chakula n.k(ni wajibu wake).

Kinachonishangaza ni namna huyu dada anavyomtreat baba mtoto wake na kila tukikutana/kuonana hachoki/hakomi kusema mume wangu/baba fulani akinioa nitafanya hivi mara nitafanya vile(jamaa hana mpango nae zaidi ya kulea mtoto alishafanya uamuzi wa kutokumuoa kutokana na tabia zake), kiukweli huwa nabaki namsikitikia tu maana mwanaume mwenye utimamu wa akili hawezi kuoa mwanamke mwenye tabia za hovyo kiasi hiki. Umezaa na mwanamke lakini kila siku ni matukio, ukinyanyua simu kumpigia au kupokea ni matukio tu hayaishi leo hili kesho lile . Kwa tabia hizi baadhi kama za huyu dada naziorodhesha hapa chini kwanini usiwe single mother milele?

  1. Unamgeuza mtoto kuwa njia ya kipato chako&mtaji, hii ipo sana kwa wanawake wengi wanatumia watoto kama chanzo cha kupata pesa. Mahitaji ya muhimu ni haki kwa mtoto ila ukizidisha miamala ni upigaji kama upigaji mwingine. Kila siku ni kuomba hela wiki nzima unadanganya mtoto anaumwa na haumwi na sababu nyinginezo nyingi na hela ikishapatikana ni bando tu kucha kutwa kushinda tiktok na instagram. Hapa hata nilipwe mshahara ili nimuoe mwanamke wa hivi sioi.
  2. Unamtukana na kumfokea baba mtoto wako, huku ni kukosa heshima. Hili ndio lililonifanya nilete ili bandiko, hivi mwanamke mwenye heshima na unaitaka ndoa unaanzaje kumtukana mwanaume? Unamwambia mwanaume acha Useng3 we ms3nge tuma hela mtoto anaumwa na ni mzima kabisa kisa tu umelala huna bundle alafu unategemea huyo baby dady ndio aje akufanye mke? Kuna wanaume wanataabika sana kisa hawa watoto.
  3. Hutaki kufanya chochote/ kujishughulisha, mwanaume anajibana anakufungulia biashara hutaki kufanya mpaka inakufa unachotaka ni kukaa tu kuwa goli kipa. Ni kushinda mtandaoni tu na kuzurura kwenye events ambazo hazina umuhimu wowote ule.
  4. Wivu wa kipuuzi uliopitiliza, ukipiga simu isipopokelewa au ikiwa inatumika ni ugomvi na maneno ya hovyo kama vile ulikuwa na wanawake zako wengine wa huko na kujinunisha wiki nzima.
  5. Mazoea na wanaume, hii ni kujirahisisha kila mwanaume unamlilia shida zako tena kwa kumkandia baba mtoto kuwa hajali na haudumii chochote.
  6. Endeleza tabia nyinginezo zinazochangia wimbi la single mothers
Kwa tabia hizo nambariki mwamba kwa uamuzi aliouchukua nitoe angalizo kwa wanaume wenzangu tuwe makini starehe ya siku moja isijetugharimu maisha yetu yote, sio kila mwanamke ni wakupita nae tena pekupeku.

Kwenu wanawake mnaofanya haya ya kufanana na hayo alafu mnategemea kuolewa hivi mtu uko timamu kabisa unafanya mambo ya hovyo kama hayo alafu unakaa unasubiri kuolewa kabisa na unamuomba Mungu kabisa akubariki kwenye hilo?

Swali fikirishi. Kwa tabia alizonazo dada yako/zako ukiambiwa uoe mwanamke mwenye tabia zinazofanana na zake utaoa? Au ndio utajoin group la KATAA NDOA?

NAWASILISHA....

View attachment 2688750
sintokuja kuoa mwanamke mwenye mtoto mtu asiguse coment yangu.
 
kuna wengine hawana shida mkuu na kaburi la mumewe lipo anakuoneshah! Ila walio wengi hawajatulia usije ukajaribu

kuna wengine hawana shida mkuu na kaburi la mumewe lipo anakuonesha
ndo mpaka tufanye uhakiki maana wengi tabia zao hatuzijui mwanzo wanakuwaga wapole mno oa sasa uone kazi ilivyo.
 
Leo nilikuwa instagramu kwa wanaotumia huu mtandao, kwenye page ya wasafi FM wameongelea mada ya wanawake wanaozaa na waume za watu, nikataka kujua maoni ya watu juu ya hili ikabidi nisome comments….. mh!

Kama tunadhani kuna wanawake wanafanya efforts zozote kuepukana na hili wimbi la usingle mother then tunatakiwa tufikirie tena.

Kwa ujumla ni kuwa hawajali, na hawana mpango wa kujali, labda tuko kwenye dunia ya hivyo, tunawafikiria wasiojifikiria, wasiofikiria future ya watoto wao, wasiofikiria mustakabali mzima wa malezi ya watoto wao…….etc

Mtu anasema kabisa kuwa nikimpenda mwanaume nazaa tu, tukutane kwenye urithi 😂 unamfikiria huyu anaelewa kweli anachokiongea?
 
Leo nilikuwa instagramu kwa wanaotumia huu mtandao, kwenye page ya wasafi FM wameongelea mada ya wanawake wanaozaa na waume za watu, nikataka kujua maoni ya watu juu ya hili ikabidi nisome comments….. mh!

Kama tunadhani kuna wanawake wanafanya efforts zozote kuepukana na hili wimbi la usingle mother then tunatakiwa tufikirie tena.

Kwa ujumla ni kuwa hawajali, na hawana mpango wa kujali, labda tuko kwenye dunia ya hivyo, tunawafikiria wasiojifikiria, wasiofikiria future ya watoto wao, wasiofikiria mustakabali mzima wa malezi ya watoto wao…….etc

Mtu anasema kabisa kuwa nikimpenda mwanaume nazaa tu, tukutane kwenye urithi 😂 unamfikiria huyu anaelewa kweli anachokiongea?
kuna baadhi ya single moms wamejitakia kuwa hivyo na hawajali chochote kwa kuwa n maamuzi yao hasa hao wanaozaa na waume za watu, hao wanachowaza ni mali tu sio kingine sasa hapo mtoto atapata malezi gani kama sio ya hovyo?
sasa hivi hili ni janga kubwa nafanya kazi na wadada wa5, wa4 ni single moms na vitabia vyao ni vya hoooovyo kweli hata mimi nisingeweza kuvumilia.
 
ila tambua kuna tabia za wanawake zinakuja baada ya kupata mtoto ,hapa anakuwa na confidence za ajabu na kuona kwamba mtoto ndo kila kitu kwake na msaada wa baadae..

Mwanamke au mwanaume anaweza kudate na mtu akiwa na shauku ya kupata mtoto ila baada ya kupata ,anakuja kutambua kwamba tabia za mwenza wake ni mbaya na kama shida yake kamaliza ya mtoto.
Hili nalo lina ukweli wake

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Screenshot_20230716_091501_Chrome.jpg


Binafsi huwa sipendi kabisa kabisa mno mwanamke mwenye mazoea na wanaume hata akiwa ni girlfriend tu achana na mke. Eti mwanamke ana rundo la male besties; na wote anabebishana nao; na hata kuwatembelea/kutembelewa na kuonana nao physically pamoja na kupewa pesa.

Hizi ni red flags ambazo ukizipuuzia zitakuja kukugharimu sana huko mbele ya safari maana kusema kweli hakuna urafiki wa bure bure tu kati ya mwanamke na mwanaume ambaye siyo ndugu wa karibu. Mwanaume anakupa pesa kisa eti ni male bestie na asitegemee cho chote kutoka kwako? We ulisikia wapi?

Matokeo yake unakuja kugundua kuwa hawa ma male besties wake kumbe baadhi yao, kama siyo wote, huwa wanamla.

Huwa inauma sana hasa kama binti unamkubali na una mipango naye ya muda mrefu. Siwalaumu wanaoishia kukimbia japo binafsi sitakaa nikimbie jukumu takatifu la kulea kiumbe kimalaika nilichoshiriki kukileta hapa duniani tena bila ridhaa ya chenyewe. Hata mamake awe pasua kichwa namna gani tutapambana hivyo hivyo tu!
Screenshot_20230413_102909_Telegram.jpg
 
Back
Top Bottom