Mungu ibariki CHADEMA.
Ni wapumbavu tu wasio jua umuhimu wa Wapinzani Nchi hii.

Hawa panya wangesha tumaliza.
 
Habari wanajf, kama ilivyo kawaida yangu kuelezea kinagaubaga habari za mgombea wetu lissu.

Chadema tulikuwa na ngome nyingi sana ambazo tuna uhakika kama mashambulizi yakifanyika basi tutapata kura nyingi sana.

Lakini katika hizo ngome ninaona kabisa mwaka huu hali haipo vizuri kwa kuwa mapokezi ya mgombea wetu hayakuwa mazuri kabisa.

Mfano siku ya jana mgombea wetu alitakiwa kufanya mkutano kwenye jimbo la chalinze, lakini nimeshtushwa sana muitikio wa watu kwenye mkutano.

Inawezekana watu wa chalinze hawakupata habari au basi tu wameamua kutupuuzia.
Mkutano ulipangwa ufanyike saa 6 mchana, lakini cha kushangaza kabisa hadi muda huo kulikuwa hakuna watu kabisa uwanjani jambo ambalo pengine lilipelekea mgombea wetu kuhairisha kufanya mkutano hapo chalinze.

Ila ninaomba chama chetu chadema waandae mkutano mwingine hapo chalinze na watu wajulishwe mapema sana, matangazo yawepo kila sehemu ili kuvuta watu wengi waje kwenye kampeni zetu, bila kufanya hivyo tutakuwa tunapaka rangi upepo.

Chama kinatakiwa kufanya maandalizi makubwa ya mikutano ili kuondoa aibu tunazopata, mfano leo mgombea wetu yupo morogoro lakini hadi sasa hivi hakuna kinachoendelea huko morogoro.

Chini hapa ni picha za hali ilivyokuwa chalinze, watu walikuwa wachache tu ambao ni viongozi tu wa chama chetu, cha kushangaza watu walikuwa wanapita mbali kabisa na eneo la mkutano kana kwamba hakuna kinachoendelea

Picha za tukio
 
Aksanteeee! Jana tulisononeka sana. Ee Mungu we.
 
Mkumbusheni Lissu.sikuhizi anaanza kisahau kuomba kura za kipigwa risasi 16[emoji23]
 
Nilikuwa nasubiri kusikia Kama huyu poyoyo wenu Salum Mwalimu nae ataingia kwenye maonesho. Sasa tusubiri nyomi huko same Kama ya Tanga.
 
Mzee wa copy and paste ameitisha Press Conference leo ninasikia.
 
Moderator unataka habari zote za Lissu ziwekwe kwenye uzi huu siyo ? huu udikteta umeanza lini na una maana gani ? umefanya kosa kubwa sana la kiufundi
 
Mungu mbariki Moderator .
Kimsingi Moderator nishamtilia shaka , haiwezekani habari zote za uchaguzi za Lissu aweke kwenye uzi mmoja , au labda aseme hazitaki habari za Lissu , kiuhalisia haiwezekani kurundika taarifa za miezi 3 tena za maeneo tofauti kwenye uzi mmoja , huu ni udikteta wa kumshinda hata Magufuli
 
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CHADEMA anayepata sapoti kubwa kutoka kwa wazungu Tundu Lisu amekiri wazi kuwa kuishinda ccm siyo jambo rahisi hasa ikiwa chini ya uongozi wa rais Magufuli ambaye ni mwamba kweli kweli.

Tundu Lisu amewaomba wana chadema wakeshe wakiomba kwani CCM ni imara kweli kweli na wametekeleza ilani yao kwa ufanisi.

mkubwa.
 
Kazi kwa vile ccm wanatumia dola kutawala! Live coverage ipo kwa ccm tu! Mabango ccm hawataki upinzani waweke! Kutwa kutunga visheria vya hovyo kudhiti upinzani
 
Watu wengi hupenda kuungana na ambaye huwa ana shinda ili kuwa salama ki- psychology
 
unaficha jina la gazeti unazani hatulijui kua ni lile gazeti la kupanguzia mavi?
 
Hilo wanalijua . Na hata sasa wanaona jinsi mikutano inavyodolola.

JPM akija hapo Moro Hadi wataomba poo.. kisingizio Chao ni Maloli sijui.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…