Ukipita sehemu Lisu alizopita kampeni ukiwauliza waliohudhuria kuwa Lisu alisema Nini wanasema hawakumbuki

Anayebisha apite sehemu Lisu alipita awaulize Lisu aliongea nini atashangaa majibu atakayopata Ni kuwa hawakumbuki

Kazi ipo
 
Pamoja na kwamba vituo vyote vya TV hapa nchini vinammulika Magufuli na magazeti. Lakini moto wa Lissu kupitia mitandao ya kijamii ni zaidi. Najiuliza Kama vyombo habari vingetoa uwiano ulio sawa wa kurusha habari zao, Lissu angekuwa amemaliza CCM mapema kabisa.

Japo Kama kwa kupitia mitandao bado mishale yake imekuwa ni ya sumu kali kwa CCM.
 
Magufuli hana hotuba , anachokitoa ni amri za Ubabe! udikiteita! amri za Ufalme etc Hana hotuba maana hana intellect ya kutoa hotuba
 
Hahaha za Magufuli zina chosha, imagine tangu 2015 unasikiliza wimbo ule ule mpaka leo !

Madaraja, barabara, ndege, zinachosha sana, ndio maana wanapiga miziki kutwa nzima hotuba robo saa.
 
Tuhamasishe NEC iwarudishe wote walioenguliwa kihuni na tulinde ushindi wetu kwa nguvu zote tutashinda.
 
“Hata ninyi mapolisi mnaotupiga mnatakiwa kuongezewa mshahara” -Tundu lissu makambako.

Hahah Lissu jamani, kuna elimu anatoa kwa lugha rahisi sana alipaswa kulipwa na kila mwananchi mzalendo, Kuna faida zaidi tunazopata kwa TL kuamua kugombea urais hata kabla hajashinda.

Shime wananchi wazalendo tuendelee kuchangia kampeni za TL.
 
Ndo ujue ni kwa jinsi gani Lissu ni balaaa na moto wa kuotea mbali! Yaani wameminya vyombo vyote vya Habari kuonesha mikutano ya Lissu, wamepiga pini hadi live streaming ila shujaa aliyeponywa risasi 16 na Mungu anazidi kutakata tu. Lissu ni 🔥
 
Mitihani mingi ya shule huwa imegawanyika katika sehemu mbili, mtihani kwa vitendo ‘field’ na mtihani wa mwisho wa kuandika tunaita ‘paper work’ au ‘theory’ ambapo mara nyingi maksi za field huwa kati ya (30 - 40)% na theory huwa (60 - 70)%.

Hadi sasa Chadema wana angalau 30% ya ushindi kupitia kampeni wanazofanya, kama wameshapata 30% za field wamebakiza angalau 21% za theory wajihakikishie ushindi wa angalau 51%.

Asikwambie mtu mtihani wa mwisho wa theory huwa hautabiriki tofauti na maksi za field, unaweza kufanikiwa kupata CW ya 40% ukashindwa kupata hata 10% za theory.

Kwenye siasa ‘theory au paper work’ ni muhimu sana ikiwa ni pamoja na: Kuwatambua wapigakura ambao hawayumbi, CCM huifanya hii kwa kunakiri vitambulisho vya wanachama wao; Kuzitambua strongholds na kuhakikisha haziingiliwi; Kuwatambua wapigakura wasiotabirika (swing voters) hasa wanataka kusikia nini ili wafanye maamuzi ya mwisho; Kuandaa mawakala waaminifu; Kuyasaidia majimbo yanayotaka msaada zaidi; Kujiandaa kulinda kura; Kuandaa center ya kupokea matokeo (isivamiwe tena), mwisho kuwaandaa wafuasi wao kuyapokea matokeo.

Hiyo ndiyo paper work niisemayo, CHADEMA wanaweza kudanganywa na mahudhurio ya watu wakasahau vitu vya msingi vinavyoleta matokeo ya mwisho.

CCM ni wazoefu, wanaweza kuwapumbaza kwa kuviacha vyama vya upinzani kusherehekea mahudhurio kumbe wao wana plan B nyuma ya pazia.
 
Vipi hali yake, wanasema amedondoka jukwaani...eti kweli?
 
Tuzidishe Maombi kwake. Mungu atazidi Kumlinda Mh Tundu Lissu.
Ampe Baraka zote za Rohoni.
Azidi kuwa mwaminifu katika Taifa na nchi uliyompa.
🙏
 
Bila yeye kuweka ulinzi wake walindao wanakesha bure .
Hivyo Tumuombe Mungu azidi kutulinda sote na wagombea wote.
 
Tundu Lissu ni hazina kwa taifa. Watanzania tumlinde huyu mwamba kwa nguvu zote. Yeyote atakayetaka kumdhulu tumwangamize yeye kwanza kabla hata hajamgusa mpendwa wetu.
Kabisa, Safari hii Hatutaki Ujinga...Lissu analindwa na Mungu, analindwa na Jumuiya ya Kimataifa, analindwa na Umma wa Watanzania, Magustinho na Watu wake Wasiojulikana asogeze tena pua yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…