Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu na Salum Mwalimu
Mengine yapo mengi kweli kweli,mfano hili suala la polisi wa usalama barabarani kujificha vichakani na kupiga tochi halafu wanarusha picha kilimeta 5 limekuwa kero kubwa sana.Natamani siku moja wagongwe na Nyoka ndio watashika adabu.

Siku hizi nikitaka kwenda mkoa wowote Tanzania Bara basi lazima safari hiyo nipange usiku.
Tii sheria bila shuruti, Mtumiaji wa barabara sio wewe peke yako
 
Kuweni makini na hizo ahadi za kukopi za mfa maji,mfa maji lazima atape tape tu atakimbilia ashike chochote mradi apone.
 
Mh Lissu, Hongera kwa namna unavyoendelea na Kampeni, Wewe kwa hakika ni mbeba maono wa Taifa hili.

Lissu, kwa kuwa mgombea wa CCM anajaribu kuwaaminisha watu kuwa yeye ni mzalendo nambari moja wa nchi hii, Naomba unapozungumza jukwaani kote upitapo wakumbushe Watanzania juu ya mzalendo wetu huyu hasiyetaka kukaguliwa.

Tafadhali tukumbushe jinsi Prof Assad, CAG aliyeonyesha uadilifu wa hali ya juu alivyofurushwa katika nafasi hiyo alipohoji mambo kadha wa kadha yaliyofanywa na serikali hii.

Mungu akutie nguvu.
 
Nimejiuliza sana huyu mwamba Siasa zake anatumia Mtindo upi? Mbona hawezekani kwa Mtindo wowote wa Siasa?
  • Ukija Kisera unamkuta yeye ndio kasheheni Sera za Ukweli na Uhakika.
  • Ukija Kipropaganda kwake ndio penye.
  • Ukija Siasa za Kimatukio kwake ndio Nyumbani.
  • Ukija na Siasa za Kibabe hapa ndio Utamkubali.
  • Ukija na Siasa za Shobo, Shobo lake sio la Dunia hii.
  • Ukija na Siasa za Vitisho, unajikuta unajitisha Mwenyewe.
  • Ukija na Siasa za Nyomi, yeye wala Haitaji cha Wasanii wala cha Malori anachohitaji yeye ni Kipaza Sauti tu na Mtatulia kama kawa.
  • Ukileta Siasa za Huruma, hapa ndio huwa Patamu kuliko, yeye atawarudisha 7 September 2017 kwenye Mambo ya Risasi.
  • Ukileta Siasa za Ukichaa yeye ndio Haifai hata Milembe.
Hii ikanikumbusha Style moja Matata kwenye Masuala ya Kung fuu kwa wanaofutilia mombo ya Mikono. Style hii Inaitwa Tai-Chi Kunfuu . Sifa kubwa ya huu Mtindo wa Kimapigano ni kua Mshindani anatumia Style yako mwenyewe ya Kimapigano kukuadhibia.

Ubora wa Style hii ni kua inauwezo wa kuabsorb (Kufyonza) Mtindo wowote wa Kimapigano na kuimodify (kuiboresha ) ndani ya Skunde moja tu na Huwa ni Hatari kwa Matumizi.

Sasa Hii Ndio Mtindo wa Siasa za Mh Tundu Lissu Mshindani Lazima Akae tu, Atake Asitake.
 
Akigusia ya CAG hakika JPM atakuwa na kazi ya kujibu Ndugai yeye anachotaka ni uspika tu ndo maana alifanya kila linalowezekana bwana mkubwa afurahi
 
kukaguliwa.Tafadhali tukumbushe jinsi Prof Assad, CAG aliyeonyesha uadilifu wa hali ya juu alivyofurushwa katika nafasi hiyo alipohoji mambo kadha wa kadha yaliyofanywa na serikali hii.
wapiga kura hawahitaji kusikia mambo hayo
 
Ndugu zangu,

Haikueleweka mara moja kama watoto hawa wamefunga shule au lah. Picha inajieleza zaidi.
FB_IMG_15995861671081198.jpeg
 
😅😅😅😅😅😅
Pale Mgombea anapokosa sera.. hadi upupwu anashauriwa..

Tulieni tulieni.. na bado..
Siku zipo.. mutapokea 💉💉💉💉💉
Nabasubiri mutaanza kulia lia.. halafu mbili nane namba za silandilaidi.. 🤣🤣🤣🤣🤣💃🏽💃🏽💃🏽💃🏽💃🏽💃🏽💃🏽💃🏽

Magufuli 2020💯
 
Back
Top Bottom