Siwamilele
JF-Expert Member
- Oct 22, 2019
- 288
- 730
Jf ni mahakamani?Hata mwaka hauko sawa wameandika mwaka 20 huu sio mwaka wa 20 Ni mwaka wa 2020 kisheria Ni makosa aliyeandika hi taarifa Hana akili Ni bwege
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Jf ni mahakamani?Hata mwaka hauko sawa wameandika mwaka 20 huu sio mwaka wa 20 Ni mwaka wa 2020 kisheria Ni makosa aliyeandika hi taarifa Hana akili Ni bwege
Kumeeekucha kumeeekuuchaaaJiji la Dar es Salaam ambayo ni ngome Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo linatarajiwa kusimama kwa siku tatu kupisha uzinduzi wa kihistoria wa mgombea Urais wa Chama hicho.
Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema Tundu Lissu atazindua Rasmi kampeni zake kuelekea Ikulu ya Magogoni na Chamwino kwa siku tatu mfululizo katika Jiji la DSM.
Viongozi wakuu wa chama hicho watashiriki uzinduzi huo wa kampeni wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe Katibu Mkuu John Mnyika na Wajumbe wote wa Kamati Kuu.
Taarifa kutoka ndani ya Chadema zinasema siku ya kwanza ya Uzinduzi itakuwa Ijumaa tarehe 28/8/20 katika viwanja vya Mbagala Zakiem; Siku ya Pili ya Uzinduzi itakuwa Jumamosi tarehe 29/8/20 katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe na siku ya Tatu ya Uzinduzi itakuwa Jumapili tarehe 30/8/20 katika viwanja vya Tabata Segerea.
Tayari viongozi wa Kanda ya Pwani pamoja na mikoa ya kichama ya Ilala, Kinondoni na Temeke umeshaanza maandalizi makubwa ambapo inatarajiwa mikutano hiyo kuwa na umati mkubwa wa watu huku ikiongozwa kwa maandamano makubwa kabla na baada ya mikutano.
Itakuwa ni Mara ya kwanza kwa chama Cha siasa kuzindua kampeni kwa siku 3 mfululizo katika Jiji la Dar.
-----------------------------------------
*Chadema kuzindua kampeni Kikanda*
Imetolewa na Idara ya Uenezi Makao Makuu
Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Chadema, naomba kukutaarifu na kukualika rasmi (wewe na chombo chako cha habari) kwenye Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2020, utakaofanyika siku ya Ijumaa, Agosti 28, 2020, katika Uwanja wa Zakhiem Mbagala, jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
Ratiba ya mikutano ya uzinduzi itakuwa ifuatavyo;
i. Agosti 29, 2020, Uwanja wa Tanganyika Parkers, jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
ii. Agosti 30, 2020, Uwanja wa Tabata S/M, Segerea, jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
iii. Agosti 31, 2020, Uwanja wa Relini, jijini Arusha, kuanzia saa 400 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
iv. Sepetemba 1, 2020, Uwanja wa Furahisha, Kitangili, jijini Mwanza, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
v. Septemba 2, 2020, Uwanja wa Lubaga joshoni, Manispaa ya Shinyanga, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
vi. Septemba 3, 2020, Uwanja wa Chipukizi, Tabora mjini, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
vii. Septemba 4, 2020, Uwanja wa Uhuru, jijini Dodoma, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
viii. Septemba 5, 2020, Uwanja wa Rwandanzovwe, jijini Mbeya, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
ix. Septemba 6, 2020, Uwanja wa Sabasaba, mjini Mtwara, kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni.
x. Septemba 7, 2020, Uwanja wa Gombani, Chakechake, Pemba, kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 6.00 mchana. Uwanja wa Maisara, Unguja, kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 12.00 jioni.
Tunatanguliza shukrani zetu, tukikuahidi ushirikiano na kutarajia hivyo kutoka kwako na chombo chako kwa ujumla katika kuimarisha demokrasia nchini kwetu ikiwa nguzo muhimu ya maendeleo ya Watanzania wote.
Pamoja na salaam za Chama.
Wako katika ujenzi wa Taifa letu,
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Chadema
UmetumwaHivi wewe ni nani hapo chadema? Upo too low!
Tatizo wewe hulioni ukichimama nchale ukikimbia nkuki njaa mbayaNasikitishwa na wa Uzalendo wa TASNIA YA HABARI CHINI. Wana ripoti upande Mmoja zaidi. Tatizo nini?
Naona mnacheza na kodi zetu halafu unakuja kungaa sharubu humu mxuuuLipieni acheni porojo za kupenda vya bure
Maskini unatia huruma sasa unalia au unaongea na mbaaadoooHiyo ratiba imelenga kumsaidia Halima Mdee Tanganyika Packers na John Mrema Tabata temeke wanaenda tu kukamilisha ratiba waislamu wasione wamewabagua kwenye uzinduzi
Wagombea wengine majimbo mengine ya Chadema mtajijua
Eneo la Teneke huwa na Nuksi anguko la Chadema lilianzia temeke walitaja mafisadi Papa Mwembe yanga Temeke wakamtaja Lowasa .Lisu ndie aliandaa List ike Baada ya pale Lowasa aliingia akaichukua Chadema akaiua kisiasa kwa kushindwa uchaguzi na Slaa alitimka Na Lisu anapumulia mashine ya kisiasaCcm wakianzisha chokochoko za aina yoyote tutazijibu kwa nguvu ile ile iliyotumika kuzianzisha.
Wakimuua Akwilina mmoja wa chadema, na wao wajiandae kumpoteza Akwilina wao mmoja.
They are guilty of nothing hence have no fear. The guilty are afraid and have started to cause chaos.Siku zote Chadema inafanya kampeni za kistaarabu
Mungu ni mwema sana, ngoja nijiandae kwenda kusikiliza habari njema za ukombozi toka kwa wakili msomi mzalendo wa kweli. Habari kile kibabu fulani za mfenesi na mapapai ya korona wazipeleke kwa Mataga huko.
Mimi Niko kimara Kuna mtu kaingia mitini na hela za Basi walilokodi liwapeleke chadema wa huku kwenda mbagala mkutanoni anapigiwa simu hapokei kazimaVp huko Zakhem mbagala jaman mbona kimya
Huyo jamaa namfatilia kitambo tu...!Hahahaha nimejikuta nacheka tu.
Hawa ndio wale wajinga wanatakiwaga kumalizwa kama wezi wa kukuMimi Niko kimara Kuna mtu kaingia mitini na hela za Basi walilokodi liwapeleke chadema wa huku kwenda mbagala mkutanoni anapigiwa simu hapokei kazima
Nimecheka mbavu Sina wanapiga kelele kuwa huyo aliyekimbia na pesa za kukodi basi kupeleleka wanachama mbagala kanunuliwa na CCM!! Wakati mijitu mingine Ni mitapeli tu iwe CCM au ChademaHawa ndio wale wajinga wanatakiwaga kumalizwa kama wezi wa kuku
Mpaka sasa mambo ni moto wasubiri waione shooTukiacha ushabiki tuangalie uharisia Lissu ananguvu na ushawishi mkubwa Sana kisiasa toka amefika siasa ya Tanzania imechangamka na kuongeza mvuto, sipati picha Media zingepewa Uhuru wao Mambo yangezid kuwa moto... Binafsi mm sio shabiki wa siasa Ila uwa nikiskia kuhusu Lissu mwili unasisimka, nawatakia kila la kheri kwenye harakati zake