Baada ya kukaa kwenye ajenda za ndege na uwanja wa ndege chato kwa muda mrefu Sasa karudi kwenye swala hatari la sukari.
Anasema "Ujapandisha mishahara kwa miaka 5 lakini sukari uliikuta 1800 sasa hivi inauzwa 3,000 halafu unajiita Rais wa wanyonge.
Rais gani wa wanyonge design hii?"
Anasema kahawa kilo moja ilikuwa inauzwa 2500 mwaka 2015 Wakati anaingia madarakani halafu leo inauzwa 1100 yaani imeporomoka! halafu unajiita Rais wa wanyonge wanyonge wa wapi hawa?
Sukari uliipandisha kwa ulimi wako na kahawa uliishusha kwa ulimi wako Sasa utakuwa Rais wa wanyonge wapi?
My take: Rais atafutiwe mtu wa kumjibia hoja za Lissu maana sioni uwezo wake wa kujibu hizi hoja na graph ya Lissu kila siku inapanda hata kwa mtu asiyependa kusikia kwa vyovyote ataguswa
Uwe CCM uwe upinzani hoja za Tundu Lissu zitakugusa tu.